Friday, February 26, 2016

Jifunze upishi wa katles




 



 MAHITAJI
A. Nyama ya kusaga                           Kilo 1
B. Viazi mbatata                                
C. Giligilani
D. Vitunguu maji na swaumu, tangawizi, hoho, keroti
E. Chumvi kiasi, ndimu
F. Binzari nyembamba, pilipili manga
G. Mayai                                                         4
H. Unga wa sembe/ngano
I. Mafuta ya kupikia uyapendayo

MAANDALIZI
Hatua Ya Kwanza
Chukua nyama yako ya kusaga weka katika sufuria, weka chumvi kiasi, tia ndimu, kitunguu swaumu, tangawizi na iache ichemke. Usiweke maji hata kidogo itaiva yenyewe na yale maji maji yake na uhakikiche yale maji yamekauka kabisa. Ipua na uweke pembeni ukisubiri ipoe.

Hatua Ya Pili
Menya viazi vyako mbatata na usafishe vizuri, baada ya hapo vikate kate na uviweke kwenye sufuria yako, Tia chumvi kiasi, tangawizi kiasi, virushe rushe na uweke jikoni tia na maji kiasi, funika na acha vichemke kwa muda (ila mimi napendelea kuweka na maji kiasi ili yakaukie kabisa hua sipendi baada ya viazi kuwiva nichuje maji). Vikisha iva na hakikisha havina maji anza kuvisaga, utaendelea kusanga mpaka upate ulaini unaoutaka wewe.

Hatua Ya Tatu
Katakata hoho, vitunguu maji, keroti katika mfumo ule ule wa vipande vidogo vidogo na ukimaliza hapo chukua mchanganyiko wako wa nyama na viazi uweke katika chombo kimoja, halafu chukua vitunguu maji, hoho, keroti ulivyo katakata tia kwenye mchanganyiko wako wa nyama na viazi, tia swau yako, kamulia tena ndimu, weka na unga wa binzari nyembamba na pilipili manga, katia na giligilani zako, sasa anza kuchanganya vyote kwa pamoja. Changanya chananya mpaka utakapo ona vyote vimechanganyika vizuri. Please test mchanganyiko wako kuoma kama mambo yapo poa.

Hatua Ya Nne
Andaa sahani zako za kuwekea madonde yako ya katres zinyunyuzie unga wa sembe ama ngano itategemea wewe wataka unga gani. Waweza tumia unga wa sembe au ngano. Ukisha maliza hapo chukua mchanganyiko wako na utengeneze style uipendayo kama vidualisho, CD-style finger style yote kheri tu. Baada ya hapo utaviviringisha katika unga wako uliouchagua wewe na utapanga kwenye sahani, utarudia hivyo katika vidude vyote. Next chukua mayai yako yale manne yavunje na kutia katika chombo safi at the same time unakua ushabandika kichomeo chako jikoni na ushaweka mafuta yako. Tumia moto wa wastani . Mafuta yakishapata moto kiasi cha wewe kuridhika chukua katres zako tia katika mayai zungusha zungusha ili mayai yaingie pande zote halafu tia kwenye kikaangio chako jikoni, rudia kafanya hivyo kwa katres zote zilizo baki na ukimaliza hapo mambo yatakua poa na tayari kujisevia.

No comments:

Post a Comment